11 Agosti 2015 - 21:36
 Magaidi wa Daesh wawaua magaidi wengine 25 Syria

Wapiganaji wa kundi la kigaidi la Daesh wamewauwa kiasi cha magaidi 25 wa makundi mengine yanayolenga kuiangusha serikali ya Syria

Shirika la habari la ABNA linaripoti kuwa: Wapiganaji  wa  kundi la kigaidi la Daesh wamewauwa kiasi  cha magaidi 25 wa makundi mengine yanayolenga kuiangusha serikali ya  Syria  katika  shambulio  lililofanywa  usiku ndani  ya  eneo  lililowekwa  na  Uturuki  na  Marekani kuwa  lisilokuwa  na  shughuli  za  kijeshi  ikiwa  ni  mbinu wanazodai kuwa ni za kupambana  na  kundi  hilo la kigaidi  lenye  itikadi  kali.

Shambulio  hilo la  magari  manne  ya  mabomu lilifanyika karibu  na  mji  wa  Marea, sehemu  muhimu katika  ukanda huo  salama  unaounganisha  magaidi  katika  mji  uliogawika wa  Aleppo  na  njia  zao  za  kuwapatia  mahitaji  kuelekea katika  mpaka  na  Uturuki.

Shambulio  hilo  limekuja  huku  kukiwa  na  ishara kwamba  hatua  za  kuunda  eneo  hilo  salama katika maeneo  ya  jimbo  la  Aleppo ambalo kwa  sasa linadhibitiwa  na  magaidi wa Daesh ambao walikuwa wakipata mafunzo na misaada kutoka  Uturuki zinapata kasi.

Kundi  kubwa la  magaidi  nchini  Syria , Ahrar al-Sham, leo limekaribisha  rasmi  mpango  huo wa Marekani na Uturuki wa kutaka kuiangusha serikali halali ya Syria, likisema  ni  kwa maslahi ya  watu  wa  Syria  pamoja  na  usalama  wa Uturuki.

Mwisho wa habari/ 291